Jua Haki Zako

Dernier épisode
81 épisodes
- Utafiti wa punde zaidi uliofanywa na Kituo cha Utafiti wa Idadi ya Watu na Afya barani Afrika (APHRC) unaonyesha kuwa, Kusini mwa Jangwa la Sahara, msichana mmoja kati ya wanne anapata ujauzito kabla ya kufikisha miaka 18.
Ingawa sheria na sera katika nchi mbalimbali katika ukanda wa Afrika Mashariki zinatambua haki ya wasichana hao kuendelea na masomo hata baada ya kujifungua, wengi bado hukumbana na vikwazo vinavyowafanya washindwe kurudi darasani. - Nchini Kenya changamoto za kupata stakabadhi muhimu kama vile vitambulisho na vyeti vya kuzaliwa zingali zinashuhudiwa miongoni wa raia wake hususan kwenye jamii ambazo zinaishi kaunti za miapakani kama vile Busia ,Turkana na Mandera, hali inayoendelea kuwanyika raia hao haki zao za kimsingi na kukosa huduma muhimu za serikali . Hii leo katika makala Jua haki zako tunaangazia akina mama hao na watoto wao jimbo la Busia kwenye mpaka wa Kenya na Uganda
À propos de Jua Haki Zako
Jua Haki Zako ni makala yanayokuelimisha juu ya umuhimu wa kufahamu haki zako na sheria halali zilizomo kwenye jamii, mataifa na dunia kwa ujumla. Jua Haki Zako itakuelimisha juu ya masuala mbalimbali ya kisheria ndani ya Afrika Mashariki, Afrika na Duniani kwa ujumla.
Site web du podcast