

Kenya : Haki ya wafanyakazi nje ya nchi
19/12/2025
Katika Juhudi za raia wa Africa Kutafuta ajira nje ya nchi wengine wamejipata katika njia panda. Lakini ubalozi wa Austria nchini Kenya, unasisitiza taifa hilo ni salama kwa wafanyakazi wa kigeni. Skiza makala haya.

EAC : Haki ya matumizi ya mitandao
02/12/2025
Je unafahamu haki zako wakati unatumia mitandao? na Je unafahamu kwamba haustahili kuvuka kiwango fulani wakati unatumia mitandao? Paul Brain ni mtaalamu wa matumizi ya mitandao anafanunua masharti ya matumizi ya mitandao.

Kenya: Msimamo wa wavuvi wa Lamu kuhusu mbinu za kuvua samaki
29/11/2025
Kwa muda sasa wavuvi kutoka kaunti ya Lamu, nchini Kenya, wamekuwa wakizozana na serikali kuhusiana na mbinu za kisasa wa uvuvi kutokana na misimo wa serikali kuwataka watumie technolojia katika uvuvi. Mwaka 2016 serikali ya Kenya ilipitisha sheria ya kuwataka wavuvi kutumia mbinu za kisasa kuendesha shughuli za uvuvi lakini hili limeibua changomoto miongoni mwa wavuvu wanaosisitiza kutumia mbInu za kale kuendesha shughuli za uvuvi kutokana na sababu kadhaa. skiza makala haya kufahamu mengi zaidi.

Kenya : Ukeketaji bado changamato Africa
20/11/2025
Katika maeneo ya wafugaji wa kuhamahama nchini Kenya, mila na desturi bado zinaonekana kupewa kipaumbele kuliko elimu – hali inayowafanya wasichana kuwa katika hatari kubwa ya kukeketwa. Wasichana wengi hukatizwa masomo na kulazimishwa kufuata tamaduni zinazokiuka haki zao, huku ukeketaji ukiendelea kufanywa kwa usiri mkubwa licha ya juhudi za serikali na wadau kutoa elimu na kupiga marufuku tendo hilo. Takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) zinaonyesha kuwa ukeketaji wa wasichana na wanawake wenye umri wa miaka 15 hadi 49 bado ni tatizo linaloripotiwa nchini Kenya. Katika makala haya tunaangazia namna tamaduni hizi zimeendelea kushamiri katika jamii za wafugaji wa kuhama hama na jinsi zinavyomnyima mtoto wa kike haki yake ya kupata elimu na kuishi bila unyanyasaji.

Matumizi ya hadithi kupigania haki
17/11/2025
Katika makala haya tunangazia safari ya kutetea haki za binadamu kwa kutumia hadithi sauti moja, uzoefu, na ujasiri wa mtu kusimulia alichopitia. Tasisi ya Moth, imekuwa ikitumia hadithi kama si tu kwa mudhadha wa burudunai bali ni daraja linalounganisha ukweli wa mtu mmoja na uelewa wa dunia nzima. Hadithi nyingi ni za binafsi, lakini hisia zinazozibeba—hofu, matumaini, maumivu au ushindi—ni za ulimwengu mzima. Skiza makala haya kufahamu mengi.