PodcastsJua Haki Zako

Jua Haki Zako

Jua Haki Zako
Dernier épisode

61 épisodes

  • Jua Haki Zako

    Kenya: Mchakato wa kutoa taarifa za rushwa kwa tume ya EACC

    23/02/2026
    Nchini Kenya tume ya kupambana na rushwa EACC imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha mali ya umma haiporwi.
    Ila ni mchakato upi mtu anastahili kufuata kutoa taarifa kwa tume.
    Benson Wakoli alikiti chini Kipsang Sambae afisa wa EACC, tawi la Nakuru kufahamu mchakato wa kutoa taarifa kwa EACC.
  • Jua Haki Zako

    Haki ya kuhifadhi taarifa za Siri

    09/02/2026
    Je unafahamu kuhusu haki ya taarifa zako za siri kuhifadhiwa? na je unatambua hatua unazostahili kufuata iwapo zitatolewa?
    .
  • Jua Haki Zako

    Human Right Watch : Haki zinakandamizwa pembe ya Africa

    09/02/2026
    Makala haya yanaangazia ripoti  ya Human Rights Watch iliyochapishwa tarehe 4 Februari 2026, inayozungumzia hali ya kutisha ya haki za binadamu katika eneo la Pembe ya Africa.
    Ripoti hiyo inaonyesha kuwa raia wa Sudan, Sudan Kusini na Ethiopia ndio wanaobeba mzigo mkubwa wa vita vya silaha vinavyoendeshwa kwa ukatili, ambapo pande zinazopigana mara nyingi hulenga raia kimakusudi.
    Human Rights Watch inasema mashambulizi haya dhidi ya raia yamekuwa jambo la kawaida, huku wahusika wakikosa kuwajibishwa.
    Kufahamu mengi skiza makala haya.
  • Jua Haki Zako

    Kenya: Hatua za kutafuta haki kwa dhulma za kinadada mtaani Mathare

    27/01/2026
    Kwa miaka mingi Beatrice Karole amekuwa akijitolea kuhamasisha jamii kuhusiana na hatua za kuchukua wakati wanapokabiliana na unyanyasaji wa jinsia. Akiwa na shirika la kinamama la Wanawake Mashinani Initiative katika eneo la Mathare Jijini Nairobi, amefanikiwa kuwaokoa jumla ya wanawake na watoto 30 katika mwaka 2025 ambao anajivunia kuwa licha ya kunyanyaswa, walipata haki yao.
  • Jua Haki Zako

    Kenya: Wakulima wadogowadogo washinda kesi ya Sheria ya Mbegu na Mimea dhidi ya KEPHIS

    25/01/2026
    Nchini Kenya, Sheria ya Mbegu na Mimea (The Kenya Seed and Plants Varieties Act), ambayo ilitishia kuwatoza faini na kuwafunga jela wakulima wadogo kwa kugawana mbegu ambazo hazijaidhinishwa, iliamuliwa kuwa kinyume cha katiba.
    Mahakama ya Kikatiba katika kaunti ya Machakos nchini Kenya ilitoa uamuzi wa kihistoria Novemba 27 2025 kuhusu uhalali wa Sheria ya Mbegu na Aina za Mimea.
    George Ajowi amekuwa akifuatilia kesi hii na kuandaa taarifa ifuatayo.

À propos de Jua Haki Zako

Jua Haki Zako ni makala yanayokuelimisha juu ya umuhimu wa kufahamu haki zako na sheria halali zilizomo kwenye jamii, mataifa na dunia kwa ujumla. Jua Haki Zako itakuelimisha juu ya masuala mbalimbali ya kisheria ndani ya Afrika Mashariki, Afrika na Duniani kwa ujumla.
Site web du podcast
Applications
Réseaux sociaux
v8.7.0 | © 2007-2026 radio.de GmbH
Generated: 2/25/2026 - 9:06:48 AM