PodcastsJua Haki Zako

Jua Haki Zako

Jua Haki Zako
Dernier épisode

54 épisodes

  • Jua Haki Zako

    Kenya : Ahadi ya serikali kwa jamii za wachache

    23/12/2025

    Kila disemba 18 dunia huadimisha siku ya  Kimataifa ya Jamii za Walio Wachache  siku inayolenga kuzikumbusha serikali na jamii wajibu wa kulinda haki, heshima na ushirikishi wa makundi ambayo kwa miaka mingi yamekuwa yakidai kuachwa nje mipango ya serikali Nchini Kenya, jamii za walio wachache, zikiwemo jamii za wafugaji wanaohamahama, zimekuwa zikidai hazitambuliwi kikamilifu, kukosa huduma za msingi, na kutengwa katika maamuzi muhimu ya kitaifa. Makala haya yanaangazia mipango ya serikali ya Kenya kwa jamii hizo.

  • Jua Haki Zako

    Mpango wa kidijitali uliokwama unavyowanyima wanafunzi elimu ya kisasa Kenya

    21/12/2025

    Mwaka 2016, Serikali ya Kenya ilizindua Mpango wa Mafunzo kwa Njia ya Kidijitali (DLP), ikiahidi kubadilisha elimu ya msingi ya umma kupitia teknolojia. Awamu ya kwanza ikigharimu walipa kodi zaidi ya Shilingi bilioni 30, huku kukiwa na mpango wa kupanua mradi huo kwa makadirio ya Shilingi bilioni 64. Takribani miaka kumi baadaye, mpango huo unazidi kukabiliwa na matatizo makubwa na hatimaye kukwama hivyo kuwanyima wanafunzi wa shule za msingi haki zao za kupata elimu ya kidijitali.Sikiliza

  • Jua Haki Zako

    Kenya : Haki ya wafanyakazi nje ya nchi

    19/12/2025

    Katika Juhudi za raia wa Africa Kutafuta ajira nje ya nchi wengine wamejipata katika njia panda. Lakini ubalozi wa Austria nchini Kenya, unasisitiza taifa hilo ni salama kwa wafanyakazi wa kigeni. Skiza makala haya.

  • Jua Haki Zako

    EAC : Haki ya matumizi ya mitandao

    02/12/2025

    Je unafahamu haki zako wakati unatumia mitandao? na Je unafahamu kwamba haustahili kuvuka kiwango fulani wakati unatumia mitandao? Paul Brain ni mtaalamu  wa matumizi ya mitandao anafanunua masharti ya matumizi ya mitandao.

  • Jua Haki Zako

    Kenya: Msimamo wa wavuvi wa Lamu kuhusu mbinu za kuvua samaki

    29/11/2025

    Kwa muda sasa wavuvi kutoka kaunti ya Lamu, nchini Kenya, wamekuwa wakizozana na serikali kuhusiana na mbinu za kisasa wa uvuvi kutokana na misimo wa serikali kuwataka watumie technolojia katika uvuvi. Mwaka 2016 serikali ya Kenya ilipitisha sheria ya kuwataka wavuvi kutumia mbinu za kisasa kuendesha shughuli za uvuvi lakini hili limeibua changomoto miongoni mwa wavuvu wanaosisitiza kutumia mbInu za kale kuendesha shughuli za uvuvi kutokana na sababu kadhaa. skiza makala haya kufahamu mengi zaidi.

À propos de Jua Haki Zako

Jua Haki Zako ni makala yanayokuelimisha juu ya umuhimu wa kufahamu haki zako na sheria halali zilizomo kwenye jamii, mataifa na dunia kwa ujumla. Jua Haki Zako itakuelimisha juu ya masuala mbalimbali ya kisheria ndani ya Afrika Mashariki, Afrika na Duniani kwa ujumla.
Site web du podcast
Applications
Réseaux sociaux
v8.2.1 | © 2007-2026 radio.de GmbH
Generated: 1/5/2026 - 4:41:13 AM